Wednesday, October 21, 2009

SOMO LA SITA (VYAKULA NA MAPISHI)

Baada ya somo hili ni lazima:

(1) Ufahamu kuagiza chakula katika mahoteli na mikahawa utakapotembelea Afrika Mashariki

(2) Kutoa maelekezo na kupika angalau chakula kimoja cha Afrika Mashariki

=> Soma maelezo ya jinsi ya kupika pilau (uk. 103). Fanya zoezi linalofuatia.

=> Chagua chakula kimoja cha Kimarekani au Kiafrika na uelezee mahitaji na hatua za kufuata wakati wa kukiandaaa.

=> Fanya zoezi la Kumi na moja (Zoezi la Kusoma na Kuandika uk 104-105).

Methali: Pilipili usiyoila, yakuwashia nini?

Kitanza ulimi: (1) Wali wa liwali huliwa na wanawali, wasio wanawali hawali wali
(2) Waacheni wali wale wale wali wao

MAPISHI YA VYAKULA MBALIMBALI (RECIPES): BISKUTI YA CHOKOLETI (NA KYLIE)

Mahitaji:

-Unga wa ngano vikombe viwili

-Hamira kijiko cha chai moja

-Chumvi kijiko cha chai moja

-Siagi vikombe moja

-Sukari vikombe moja

-Sukari hadharani vikombe nusu

-Mayai makubwa mawili

-Chokoleti vikombe viwili


Kuandaa Biskuti na Chokoleti:


-Uchemshe jiko katika 190C

-Uongoze unga wa ngano, hamira, na chumvi katika bakuli

-Halafu uongoze siagi, sukari, sukari hadharani, na mayai katika bakuli nyingine na changanya

-Uongoze bakuli la kwanza katika bakuli la pili na changaya

-Uchanganye chokoleti na kila kitu

-Uweke mchanganyiko katika chombo

-Oka kwa dakika kumi na tano

-Halafu kula

MAPISHI YA VYAKULA MBALIMBALI (RECIPES): BIRIYANI (NA PRIYA)

"Recipes" hizi ziliandaliwa na wanafunzi. Walipika vyakula hivi na kuvileta darasani na darasa lote lilivila na kujadiliana.
  • A. Mahitaji:
  1. Mchele vikombe viwili
  2. Maji vikombe sita
  3. Nyama ya kuku kilo moja bila mifupa
  4. Vitunguu saumu vitatu (three cloves)
  5. Nyanya moja kubwa
  6. Kitunguu kimoja kikubwa
  7. Tangawizi
  8. Masala ya biriyani vijiko vinne
  9. Pilipili mbili
  10. Pilipili hoho ya kutosha
  11. Chumvi ya kutosha
  12. Mafuta
  • B . Mchanganyiko:

  1. Katakata kuku vipande vidogo halafu osha katika maji moto.
  2. Changanya kitunguu saumu, pilipili, pilipili hoho, tangawizi, chumvi kijiko kimoja na mafuta robo kikombe katika “blender” na changanya mpaka iwe mchanganyiko mzuri sana.
  3. Changanya mchanganyiko na kuku pamoja katika sufuria au “zip lock bag” na ni lazima“umarinate” kuku kwa masaa matatu au manne.

  • C. Biriyani:

  1. Katakata kitunguu na nyanya vipande vidogo.
  2. Washa moto na ongeza mafuta kwenye sufuria halafu kaanga kitunguu na nyanya vizuri sana.
  3. Ongeza kuku na mchanganyiko katika sufuria.
  4. Changanya vitu hivi vyote kwenye sufuria vizuri sana.
  5. Osha mchele na maji moto, halafu baada ya kuosha ongeza mchele na maji vikombe sita katika sufuria
  6. Ongeza chumvi ya kutosha na masala ya biriyani vijiko vinne.
  7. Changanya vitu hivi vyote kwenye sufuria vizuri sana.
  8. Kisha funika chakula na gazeti na kifuniko ili mvuke usitoke.
  9. Wacha chakula kijipike kwa muda wa kama nusu saa hadi kimeiva.
  10. Epua na pakua baada ya kupoa.

Tuesday, October 20, 2009

CHANDARUA CHA MBU

















Mama na mtoto wake mdogo wanatumia chandarua ili kujikinga na mbu

TOVUTI JUU YA MAGONJWA MBALIMBALI

Tafadhali sana tazameni tovuti hizi ili mpate habari juu ya magonjwa mbalimbali:

Friday, October 9, 2009

KARATA YA MZUNGU WA NNE

INSHA YA TATU - ILETWE DARASANI JUMATATU (12/10/2009)

AMA

Jibu maswali katika wimbo wa Mume Bwege. Majibu yako ni lazima yawe katika insha tafu fupi fupi zenye nusu ukurasa kila moja. Unaweza kuleta insha yako darasani Jumatatu au kuiweka katika blogu moja kwa moja kama maoni (comments)


Au

Andika insha ndefu (ukurasa mmoja na nusu) kuhusu makazi yako. Andika kila kitu kuanzia historia yako fupi - ulizaliwa wapi, nyumbani ni wapi, kama unapapenda, sasa unakaa wapi, kwa nini, unapenda kusafiri kwa njia gani, toa maelekezo ya watu kufika nyumbani kwako hapa Gainesville au nyumbani kwa wazazi wako. Hii ni insha ya jumla na lengo lake kuu ni kuhakikisha kwamba unajua kutoa na kufuata maelekezo (to give and follow directions). Be creative and try using any grammar that we have seen so far. Hapana shaghalabaghala!

Wednesday, October 7, 2009

MUME BWEGE (NA BUSHOKE - MWANAMUZIKI WA BONGO FLEVA KUTOKA TANZANIA)



Tazama video hii na soma maneno ya wimbo (lyrics)












MUME BWEGE (NA BUSHOKE – TANZANIA)

Maneno yamewekwa hapa na darasa la Kiswahili la mwaka wa pili

Chuo Kikuu cha Florida, Gainesville


Nilikuwa na mpenzi wangu

Nani asiyemjua

Mtoto kaumbika

Utasema malaika

Miezi kadhaa ikasogea

Mtoto (wa) kwanza tukazaa

Mtoto katoka Mwarabu

Swali lilikosa jibu

Akasema we hujui

Mtoto kafata kwa babu

Nikagunaguna pale mzee nikauchuna


Mtoto (wa) pili tukazaa

Huyu wa sasa Mchina doh

Nikasema mama vipi

Mbona mi sielewi

Akasema we hujui

Huyu kafata kwa bibi


Aa wewe mama wee

Ingekuwa ungefanyeje


Mwenzenu nalala chini

Mke wangu kitandani

Nikilala kitandani

Kila mtu shuka lake

Mwenzenu nalala chini

Mke wangu kitandani

Nikilala kitandani

Basi ujue mzungu wa nne


Nikiuliza kwa nini

Anasema amenipa likizo eeh

Siyo kama napenda

Imenilazimu ooh

Siyo kama napenda

Ananilazimisha yoo


Mwenzenu naosha vyombo

Mwenzenu napiga deki

Mzee mzima napika

Jamani nafua nguo

Siyo kama napenda

Nalazimishwa mimi


Lo, hii sasa kali

Jana kaniambia anataka kwenda klabu na marafiki zake

Ila kaniambia mimi

Nilinde nyumba eti wezi wasije wakaiba

Eee Bize Man hii halali kweli

Oyaa Mbiye njoo unisaidie huku nyumbani mwenziyo naonewa

Chifu Rumanyika, unajifanya hujui

Ooo naonewa mimi

Aa wewe mama wee

Ingekuwa ungefanyeje


MSAMIATI


-jua - fahamu

umbika - naturally attractive

mzungu wa nne - opposite direction

likizo - mapumziko

lazimu - ni lazima

lazimisha - force to do something

osha - wash

vyombo - dishes

piga deki - kusafisha sakafu

fua nguo - wash clothes

linda - protect

wezi - wingi wa mwizi

iba - steal

halali - fair

onea - mistreat

=======================================

MASWALI:

Baada ya kutazama video hii na kusoma maneno ya wimbo huu:


(1) Andika tofauti za kitamaduni kati ya wanaume wa Kitanzania na wanaume wa Kimarekani. Ni lazima utumie kauli ya kutendea (prepositional form) mf. pika - pikia, soma - somea n.k.

Mfano: Kwa kawaida wanaume wa Kitanzania hawajipikii chakula lakini wanaume wa Kimarekani wakati mwingine wanajipikia chakula chao

(2) (Kwa wavulana/wanaume au jifanye (pretend) kuwa mwanaume), kama wewe ungekuwa ndiye unayeimbwa katika wimbo huu ungefanya nini?

(3) Umeupenda wimbo huu? Kwa nini?

Friday, September 11, 2009

LEO NI TAREHE 11/9/2009

=> Ulikuwa wapi siku tarehe 11/9/2001? Unakumbuka nini?

=> Ungekuwa rais wa Marekani wakati ule ungefanya nini? Ungeenda kupigana vita Afghanistan na Iraq?

MAZOEZI YA -NGE-, -NGALI- NA -NGELI-

Tazama picha zifuatazo na chini yake uandike mambo ambayo ungefanya na yale ambayo usingefanya kama ungekuwa wewe.

(1) Barack Obama -Raisi wa arobaini na nne wa Marekani













(2) Rush Limbaugh - Mtangazaji wa redio ya kihafidhina



















(3) Machen - Rais wa chuo Kikuu cha Florida



















(4) George Bush - Rais wa arobaini na tatu wa Marekani



















(5) Wewe - kuna kitu cho chote ambacho unafikiri kwamba ni afadhali usingekifanya?