Wednesday, September 10, 2008

MARAISI WA TANZANIA

MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE
Raisi wa kwanza. Alikuwa raisi mwadilifu aliyeipenda sana Tanzania na watu wake. Hakuwa fisadi wala mla rushwa. Wakati wake watoto wote tulisoma bure na huduma za afya zilikuwa bure pia. Ningependa kuwa kama yeye kama ningekuwa raisi wa Tanzania.



















NDUGU ALI HASSAN MWINYI
Raisi wa pili. Yeye alikuwa raisi mpole na legelege. Rushwa na ufisaidi vilistawi sana katika kipindi chake. Yeye aliitwa Mzee Rukhsa kwa tabia yake ya kusema ndiyo kwa kila kitu hata katika mambo ya rushwa. Nisingependa kuwa kama yeye kama ningekuwa raisi wa Tanzania
















MHESHIMIWA BENJAMIN MKAPA
Raisi wa tatu. Yeye ni mwanafunzi wa Mwalimu Nyerere na Nyerere alimchagua. Nyerere pengine hakumjua vizuri mwanafunzi wake kwa sababu raisi huyu anasemwasemwa kwamba alikuwa fisadi na mla rushwa. Kama ni kweli basi yeye ni raisi mbaya. Mwalimu Nyerere angekuwa hai ningemwuliza kwanini alituchagulia raisi mbaya kama huyu. Nisingependa kuwa Ben. Mkapa kama ningekuwa raisi wa Tanzania leo.
















JAKAYA KIKWETE
Raisi wa nne. Yeye ni raisi kijana na mwenye bashasha na anapendwa na watu. Kila alipohutubia alisema "Maisha bora kwa kila Mtanzania" na Watanzania wengi walimwamini. Ni miaka karibu mitatu sasa na hakuna maisha bora kwa kila Mtanzania. Ijapokuwa yeye si fisadi lakini serikali yake imeshindwa kabisa kupambana na ufisadi na rushwa ya waziwazi. Yeye ameanza vibaya lakini ngoja tuone atakavyoendelea na utawala wake. Ninampenda.



















SWALI: Ni raisi gani wa Marekani unayempenda sana? Kwa nini? Na yupi ambaye humpendi sana? Kwa nini?

1 comment:

Anonymous said...

Raisi Kikwete katika habari.

Kikwete @ USAID