Wednesday, October 21, 2009

MAPISHI YA VYAKULA MBALIMBALI (RECIPES): BIRIYANI (NA PRIYA)

"Recipes" hizi ziliandaliwa na wanafunzi. Walipika vyakula hivi na kuvileta darasani na darasa lote lilivila na kujadiliana.
  • A. Mahitaji:
  1. Mchele vikombe viwili
  2. Maji vikombe sita
  3. Nyama ya kuku kilo moja bila mifupa
  4. Vitunguu saumu vitatu (three cloves)
  5. Nyanya moja kubwa
  6. Kitunguu kimoja kikubwa
  7. Tangawizi
  8. Masala ya biriyani vijiko vinne
  9. Pilipili mbili
  10. Pilipili hoho ya kutosha
  11. Chumvi ya kutosha
  12. Mafuta
  • B . Mchanganyiko:

  1. Katakata kuku vipande vidogo halafu osha katika maji moto.
  2. Changanya kitunguu saumu, pilipili, pilipili hoho, tangawizi, chumvi kijiko kimoja na mafuta robo kikombe katika “blender” na changanya mpaka iwe mchanganyiko mzuri sana.
  3. Changanya mchanganyiko na kuku pamoja katika sufuria au “zip lock bag” na ni lazima“umarinate” kuku kwa masaa matatu au manne.

  • C. Biriyani:

  1. Katakata kitunguu na nyanya vipande vidogo.
  2. Washa moto na ongeza mafuta kwenye sufuria halafu kaanga kitunguu na nyanya vizuri sana.
  3. Ongeza kuku na mchanganyiko katika sufuria.
  4. Changanya vitu hivi vyote kwenye sufuria vizuri sana.
  5. Osha mchele na maji moto, halafu baada ya kuosha ongeza mchele na maji vikombe sita katika sufuria
  6. Ongeza chumvi ya kutosha na masala ya biriyani vijiko vinne.
  7. Changanya vitu hivi vyote kwenye sufuria vizuri sana.
  8. Kisha funika chakula na gazeti na kifuniko ili mvuke usitoke.
  9. Wacha chakula kijipike kwa muda wa kama nusu saa hadi kimeiva.
  10. Epua na pakua baada ya kupoa.

Tuesday, October 20, 2009

CHANDARUA CHA MBU

















Mama na mtoto wake mdogo wanatumia chandarua ili kujikinga na mbu

TOVUTI JUU YA MAGONJWA MBALIMBALI

Tafadhali sana tazameni tovuti hizi ili mpate habari juu ya magonjwa mbalimbali:

Friday, October 9, 2009

KARATA YA MZUNGU WA NNE

INSHA YA TATU - ILETWE DARASANI JUMATATU (12/10/2009)

AMA

Jibu maswali katika wimbo wa Mume Bwege. Majibu yako ni lazima yawe katika insha tafu fupi fupi zenye nusu ukurasa kila moja. Unaweza kuleta insha yako darasani Jumatatu au kuiweka katika blogu moja kwa moja kama maoni (comments)


Au

Andika insha ndefu (ukurasa mmoja na nusu) kuhusu makazi yako. Andika kila kitu kuanzia historia yako fupi - ulizaliwa wapi, nyumbani ni wapi, kama unapapenda, sasa unakaa wapi, kwa nini, unapenda kusafiri kwa njia gani, toa maelekezo ya watu kufika nyumbani kwako hapa Gainesville au nyumbani kwa wazazi wako. Hii ni insha ya jumla na lengo lake kuu ni kuhakikisha kwamba unajua kutoa na kufuata maelekezo (to give and follow directions). Be creative and try using any grammar that we have seen so far. Hapana shaghalabaghala!

Wednesday, October 7, 2009

MUME BWEGE (NA BUSHOKE - MWANAMUZIKI WA BONGO FLEVA KUTOKA TANZANIA)



Tazama video hii na soma maneno ya wimbo (lyrics)












MUME BWEGE (NA BUSHOKE – TANZANIA)

Maneno yamewekwa hapa na darasa la Kiswahili la mwaka wa pili

Chuo Kikuu cha Florida, Gainesville


Nilikuwa na mpenzi wangu

Nani asiyemjua

Mtoto kaumbika

Utasema malaika

Miezi kadhaa ikasogea

Mtoto (wa) kwanza tukazaa

Mtoto katoka Mwarabu

Swali lilikosa jibu

Akasema we hujui

Mtoto kafata kwa babu

Nikagunaguna pale mzee nikauchuna


Mtoto (wa) pili tukazaa

Huyu wa sasa Mchina doh

Nikasema mama vipi

Mbona mi sielewi

Akasema we hujui

Huyu kafata kwa bibi


Aa wewe mama wee

Ingekuwa ungefanyeje


Mwenzenu nalala chini

Mke wangu kitandani

Nikilala kitandani

Kila mtu shuka lake

Mwenzenu nalala chini

Mke wangu kitandani

Nikilala kitandani

Basi ujue mzungu wa nne


Nikiuliza kwa nini

Anasema amenipa likizo eeh

Siyo kama napenda

Imenilazimu ooh

Siyo kama napenda

Ananilazimisha yoo


Mwenzenu naosha vyombo

Mwenzenu napiga deki

Mzee mzima napika

Jamani nafua nguo

Siyo kama napenda

Nalazimishwa mimi


Lo, hii sasa kali

Jana kaniambia anataka kwenda klabu na marafiki zake

Ila kaniambia mimi

Nilinde nyumba eti wezi wasije wakaiba

Eee Bize Man hii halali kweli

Oyaa Mbiye njoo unisaidie huku nyumbani mwenziyo naonewa

Chifu Rumanyika, unajifanya hujui

Ooo naonewa mimi

Aa wewe mama wee

Ingekuwa ungefanyeje


MSAMIATI


-jua - fahamu

umbika - naturally attractive

mzungu wa nne - opposite direction

likizo - mapumziko

lazimu - ni lazima

lazimisha - force to do something

osha - wash

vyombo - dishes

piga deki - kusafisha sakafu

fua nguo - wash clothes

linda - protect

wezi - wingi wa mwizi

iba - steal

halali - fair

onea - mistreat

=======================================

MASWALI:

Baada ya kutazama video hii na kusoma maneno ya wimbo huu:


(1) Andika tofauti za kitamaduni kati ya wanaume wa Kitanzania na wanaume wa Kimarekani. Ni lazima utumie kauli ya kutendea (prepositional form) mf. pika - pikia, soma - somea n.k.

Mfano: Kwa kawaida wanaume wa Kitanzania hawajipikii chakula lakini wanaume wa Kimarekani wakati mwingine wanajipikia chakula chao

(2) (Kwa wavulana/wanaume au jifanye (pretend) kuwa mwanaume), kama wewe ungekuwa ndiye unayeimbwa katika wimbo huu ungefanya nini?

(3) Umeupenda wimbo huu? Kwa nini?

Friday, September 11, 2009

LEO NI TAREHE 11/9/2009

=> Ulikuwa wapi siku tarehe 11/9/2001? Unakumbuka nini?

=> Ungekuwa rais wa Marekani wakati ule ungefanya nini? Ungeenda kupigana vita Afghanistan na Iraq?

MAZOEZI YA -NGE-, -NGALI- NA -NGELI-

Tazama picha zifuatazo na chini yake uandike mambo ambayo ungefanya na yale ambayo usingefanya kama ungekuwa wewe.

(1) Barack Obama -Raisi wa arobaini na nne wa Marekani













(2) Rush Limbaugh - Mtangazaji wa redio ya kihafidhina



















(3) Machen - Rais wa chuo Kikuu cha Florida



















(4) George Bush - Rais wa arobaini na tatu wa Marekani



















(5) Wewe - kuna kitu cho chote ambacho unafikiri kwamba ni afadhali usingekifanya?

UNAWAPENDA WALIMU?

Walimu ni watu muhimu sana katika maisha yetu. Wao hutufundisha kusoma, kuandika na kuwa na adabu nzuri. Lakini mara nyingi hawalipwi pesa nyingi, wanadharauliwa na wanafanya kazi katika mazingira magumu sana hasa kule Afrika.

Ungekuwa rais wa Tanzania, ungefanya nini kuwasaidia walimu kama huyu pichani anayemfundisha mtoto mdogo kuandika namba tano?

USAFIRI WA HATARI AU?

Watoto hawa ni lazima waende shule na baba ana pikipiki moja tu na hana gari. Je, ungekuwa wewe ungefanya nini?


WATOTO WANAOFANYISHWA KAZI BADALA YA KWENDA SHULE

Una maoni gani kuhusu watoto wadogo kufanyishwa kazi ngumu badala ya kwenda shule?
















Wednesday, March 25, 2009

CHEMSHABONGO YA MWISHO - KESHO ALHAMISI TAREHE 26/3/2009

(1) Ufahamu na Insha: Someni na mfahamu kila kitu kuhusu sura ya kwanza na ya pili ya Ndoto ya Amerika. Kutakuwa na maswali mafupi ya insha kuhusu sura hizo mbili.

(2) Msamiati: Ni lazima mfahamu msamiati wote wa sehemu ambazo tumesoma na kutafsiri darasani. Utaweza kuulizwa kutafsiri, kutumia maneno ya msamiati katika sentensi au kuoanisha.

(3) Sarufi - Ni lazima ufahamu -have/has been, used to (past habitual) na past continuous tense (we were eating...) n.k.

(4) Misemo - mfano - una wazimu? Umerogwa? n.k.

Tuesday, February 24, 2009

KUHUSU MTIHANI WA KATIKATI - TAFADHALI SOMENI

Mtihani wa katikati utafanyika darasani siku ya Jumanne tarehe 26/2/2009. Mtihani utachukua saa moja na nusu. Topiki/mada za muhimu kuzingatia:

(1) Ni lazima uwe tayari kuandika insha fupifupi juu ya topiki zote ambazo tayari tumeshazisoma darasani mfano; kujistarehesha (somo la 8), Usafiri (somo la tisa), Kuwalea watoto (somo la 10), Hali ya Hewa (somo la 11) na kazi (somo la 12 - alama za ziada).

Kwa hivyo;

=> Utaulizwa maswali mafupi mfano - wewe unajistareheshaje? na utaandika insha fupi. Wewe sasa ni wmanafunzi wa mwaka wa pili na tunakutegemea kwamba unaweza kuandika insha nzuri na kujieleza kwa Kiswahili bila wasiwasi wo wote.

(2) Sarufi: Ni lazima ufahamu hu- tense negative, jinsi ya kufanya contractions, causative (sh-), conditional -ki- (positive na negative) na sarufi yote ambayo umeshasoma mpaka wakati huu. SITAKI ufanye makosa mabaya kabisa ya kisarufi kama vijana VYA, mji ya, mpenzi ya...Makosa kama haya yatakufanya upoteze pointi nyingi sana!

(3) Msamiati: Ni lazima ufahamu maneno yote kutoka zoezi la kusoma la somo la nane (Ninapenda sana kwenda ufukoni - uk 127-128) na zoezi la kusoma la somo la 10 (Malezi yangu - uk 151-152). Utaulizwa kuoanisha maneno (matching), kutafsiri pamoja na kutumia maneno hayo katika sentesi. Unaweza pia kuulizwa kutafsiri msamiati wo wote ambao tumeshaona darasani.

Huu utakuwa ni mtihani rahisi na hakuna shida ya kuwa na wasiwasi. Nitakuwa ofisini mwangu kesho Jumatano (25/2/2009) kuanzia saa sita mchana mpaka saa saba na nusu mchana. Unaweza kufika wakati huo kama una swali lolote. Unaweza pia kuniandikia e-mail kupitia profesamatondo@gmail.com. Nitakuwa nikitazama e-maili hii mara kwa mara.

Asanteni sana!
==================

Thursday, February 12, 2009

CHEMSHABONGO NAMBA TATU - SPRING 2009

(1) Usikilize tena wimbo wa Mtoto Akililia Wembe kutoka you tube aua hapa. Andika insha isiyopungua ukurasa mmoja kuhusu swali lifuatalo '...mtoto akililia wembe tumpe?" Tumia causative angalau (at least) tano. (alama 20. Ninataka insha ndefu nzuri)

(2) Wewe ukiwa na watoto siku moja, utawapa adhabu gani ili kuwaadabisha? Utawapiga? Kwa nini? Andika jibu refu kuhusu suala hili. (alama 10)

(3) Fanya zoezi la tatu (ukurasa wa 154) katika kitabu chako. Kabla hujajibu swali hili, ni lazima kwanza utembelee hapa. (alama 13)

(4) Je, katika sikukuu hii ya Wapendanao utafanya nini? Andika insha fupi. (alama 10)

MUHIMU: Majibu ya swali la pili ni lazima yawekwe hapa kama maoni (comments). Majibu ya Maswali ya 1, 3 na 4 yaletwe darasani Jumanne ya wiki kesho (17/2/2009)

Thursday, November 20, 2008

MARAISI WA MAREKANI














Ni raisi yupi unayempenda sana? Kwa nini? Yupi humpendi? Kwa nini humpendi? Yeye alifanya nini?

KANGA KUSHEREHEKEA USHINDI WA OBAMA
















































Kanga hizi zinasemaje? Umezipenda?

Monday, November 10, 2008

RATIBA YA KUWASILISHA MADA DARASANI

Tafuta mada yo yote kutoka katika magazeti, redio au kutoka sehemu yo yote na uwasilishe darasani kwa muda wa dakika tano hadi kumi. Tafadhali usisome na jaribu sana kutumia maneno yako mwenyewe.

WIKI YA 12

Novemba 10- JOY

Novemba 12 - ASHLEY

Novemba 14 - TIM


WIKI YA 13

Novemba 17 - LAURA

Novemba 19 - ALISON

Novemba 21 - CECILIA


WIKI YA 14
Novemba 24 - KYLIE

WIKI YA 15
Desemba 3 - PRIYA
Desemba 5 - KELLEY

Sunday, November 9, 2008

CHEMSHABONGO NAMBA TATU (KUFANYIA NYUMBANI)

(1) Tazama video ya MUME BWEGE (Stupid husband) hapo chini na soma maneno ya wimbo (lyrics) halafu jibu maswali (1) na (3). Majibu yako ni lazima yawe katika insha.

(2) Kuna chakula cho chote unachokipenda? Andika mahitaji ya chakula hicho na kinavyopikwa. Andika kila kitu ambacho unataka watu wengine wafahamu kuhusu chakula chako.

(3) Andika sentensi kumi ndefu ukitumia relative markers katika tense zifuatazo. Sentensi moja katika kila "tense" ni lazima iwe katika ukanushi (negative)

-na-
-li-
-ta-
-me-
-mesha-
hu-

MENU KATIKA MKAHAWA WA "SHERATON"



















SWALI:
Kuna chakula cho chote ambacho unaweza kula katika mkahawa huu wa "Sheraton"? Andika mazungumzo mafupi kati yako na mhudumu kuhusu jinsi utakavyohudumiwa kuanzia mwanzo mpaka mwisho.

Thursday, November 6, 2008

WAUZAJI WADOGO WADOGO

Wauzaji hawa wadogowadogo wanauza nini? Kuna cho chote unachotaka kununua? Andika mazungumzo yako na muuzaji mmoja. Usisahau kuomba kupunguziwa bei.






MAGAZETI YA TANZANIA NA USHINDI WA OBAMA